Skip to main content

Wizara ya Maliasili yaomba bilioni 624

 Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana, ameliomba Bunge liidhinishe jumla ya Shilingi bilioni 624,142,732,000 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya sekta ya Maliasili na Utalii kwa mwaka ujao wa fedha. 

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana

Akisoma bajeti hiyo Waziri Balozi Dkt. Chana amesema wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 inatarajia kujenga barabara mpya zenye urefu wa kilomita 2,500 katika hifadhi za Taifa za Arusha, Burigi - Chato, Gombe, Katavi, Kilimanjaro, Kitulo, Mahale, Udzungwa, Manyara, Rubondo, Rumanyika - Karagwe, Ruaha, Mikumi, Nyerere na Serengeti.

Aidha, Wizara itajenga njia za utalii zenye urefu wa kilomita 251 na barabara za kutembea kwa miguu zenye urefu wa kilomita 342.5.

Waziri Chana ameongeza kuwa Wizara hiyo itawezesha uandaaji wa mipango ya matumizi bora ya ardhi katika vijiji 30 vinavyozunguka Hifadhi ya Taifa Nyerere na vijiji 18 vinavyozunguka Hifadhi ya Taifa Serengeti, kuchimba mabwawa mapya nane na kukarabati mabwawa matano kwa matumizi ya wanyamapori katika hifadhi za Taifa za Mkomazi, Tarangire, Mikumi, Katavi, Ruaha, Saadani, na Serengeti.

"Wizara itaboresha maeneo ya malisho ya wanyamapori kwa kudhibiti mimea vamizi katika eneo lenye ukubwa wa hekta 30,331 katika hifadhi za Taifa Nyerere, Saadani, Serengeti, Arusha, Ibanda-Kyerwa, Mto Ugalla, Mikumi, Mkomazi na Katavi, vilevile, Wizara itaotesha miti ya asili 100,000 katika Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro," amesema Balozi Chana.

Comments

Popular posts from this blog

NAFASI ZA KAZI MPYA UNICEF (Re- Advertisement): Temporary Appointment - Health (Financing) Specialist P3 Tanzania

APPLY NOW Job no:   576667 Contract type:   Temporary Appointment 💥 TAZAMA NAFASI MPYA UNICEF SENIOR OPERATIONS ASSOCIATIONS Duty Station:   Dar-es-Salaam Level:   P-3 Location:   United Republic of Tanzania Categories:   Health Deadline: 10 Nov 2024 11:55 PM UNICEF works in over 190 countries and territories to save children’s lives, defend their rights, and help them fulfill their potential, from early childhood through adolescence. At UNICEF, we are committed, passionate, and proud of what we do. Promoting the rights of every child is not just a job – it is a calling. UNICEF is a place where careers are built: we offer our staff diverse opportunities for personal and professional development that will help them develop a fulfilling career while delivering on a rewarding mission. We pride ourselves on a culture that helps staff thrive, coupled with an attractive compensation and benefits package. Visit  our website  to learn more about what we ...

Tangazo la Nafasi Za Kazi Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST)

  Apply Now Apply Now/Omba sasa nafasi hizi za kazi

Tech-Driven Conservation: Protecting the Congo Basin Rainforest

The Congo Basin rainforest, the world’s second-largest tropical forest, plays a crucial role in global biodiversity and climate regulation.  Spanning over 500 million acres, it is home to diverse wildlife, including gorillas, forest elephants, and rare plant species.  Additionally, the rainforest acts as a major carbon sink, helping mitigate climate change. However, illegal logging, mining, and agricultural expansion pose significant threats to this fragile ecosystem. Technology is emerging as a powerful tool in the fight against deforestation and habitat destruction.  Advanced satellite imagery and AI-powered monitoring systems are being used to track illegal activities in real time, allowing conservationists to respond swiftly to environmental threats.  Drones are also being deployed for aerial surveillance, capturing high-resolution images to assess forest health and detect deforestation hotspots. Blockchain technology is revolutionizing supply chain transparency,...