Skip to main content

Jinsi ya Kufanya Biashara ya Kuagiza Bidhaa China

 


Hello ndugu wasomaji wangu wa blogu yetu pendwa ya lusaku.com ambayo hapa huwa nashare fursa mbalimbali za kimasomo nje ya nchi na kazi hapa nchini Tanzania na Africa mashariki.

Leo nimeona nikusogezee makala itakayoelezea fursa ya jinsi ya kuagiza bidhaa kutoka China kuja Tanzania.

Awali ya yote Mimi mwandishi ninao uzoefu wa kutosha kwenye hili kwani nilifanikiwa kuenda China kimasomo mnamo mwaka 2018 Hadi 2020 ambapo nilipofika China sio kwamba nilibase kwenye masomo pekee bali nilikuwa mtu wa kujichanganya sehemu mbalimbali katika kusaka fursa mbalimbali za kujikwamua kiuchumi kama mtanzania.

Hivyo basi Leo nitakufundisha jinsi, njia au mbinu ambazo utatakiwa kuzitumia ili uweze na wewe kufanya biashara ya kitu chochote kuagiza kutoka China kama wengine wanavyoweza kufanya hivyo mfano wafanyabiashara wengi wa kariakoo kama vanjabei, na wengine wengi wanachukua mizigo kutoka nje haswa China ingawa Kuna wengine wanachukua nchi tofauti kama uturuki, Dubai ,India n.k.

Zifuatazo ni njia za jinsi ya kufanya biashara ya kuagiza bidhaa kutoka China:-

1. Aina ya bidhaa unayotaka kununua kutoka China. 

Hii inaweza kuonekana ni kawaida lakini ni muhimu kwa sababu itakusaidia kujua wapi utaipata maana China Kuna masoko makubwa kama mawili Moja ndio hili tunalolifahamu wengi wetu linaitwa Guangzhou na lingine Linaitwa Yiwu, hivyo kama utahitaji kuenda mwenyewe direct kufunga mzigo basi ufahamu aina za hayo masoko na bidhaa zinazopatikana kiurahisi huko kwenye haya masoko itakurahisiahia kwa sababu haya masoko hayapo karibu karibu hivyo unahitajika kusafiri na kutumia gharama zingine ukiwa ndani ya China. Hivyo kufahamu aina ya bidhaa ni muhimu. Mfano elektronik kama simu, tv, blender utavipata Guangzhou.

2. Supplier/ manufacturer (muuzaji au kiwanda)

Hawa ndio wauzaji wenyewe wa jumla kama ni duka kubwa lililopo kule China au mtengenezaji mwenyewe ambayo ni nzuri zaidi. Hii ni point muhimu sana kujua na ukiwa na contacts kadhaa za wauzaji waaminifu kutoka China , utaepuka gharama za kuenda mwenyewe China na utakachotakiwa kufanya ni kumtumia pesa huyo muuzaji mfano supplier wa simu smart phones ambayo yupo Guangzhou utamtumia pesa then atakufungia mzigo na kukutumia. Kwenye point zifuatazo naelezea jinsi ya kutuma mzigo na kufanya malipo ya mzigo wako.

3. WeChat App (Njia kuu ya mawasiliano China)

Hii nayo ni muhimu mno kuwa nayo, kwa sababu hakuna njia nyingine ambayo ni rahisi kama WeChat , hapa utaweza kuwasiliana na supplier wako Moja kwa Moja wakati wowote kwa lugha ya kiingereza na akakuelewa bila shida yoyote kwani WeChat App Ina uwezo wa kutafsiri meseji zote utakazo kuwa unamtumia supplier wako, pia nilisema unaweza kulipia mzigo wako ukiwa hapa hapa Tanzania, yes, Kuna kitu kinaitwa WeChat pay ambapo utaweza kuweka pesa zako kwenye WeChat wallet na ukafanya transaction za pesa hata kama haupo China au hii ikiwa ni ngumu basi Kuna bank transfer ambapo utaweza kumtumia pesa, hakikisha umejirudhisha na supplier wako kwa kuuliza watu mbalimbali ambao wameshawahi kununua bidhaa kutoka kwa huyo muuzaji na kwamba ni muaminifu, hiyo itakusaidia kutopoteza mzigo wako muda na pesa.

4. Agent wa kusafirisha mizigo Yako.

Hapa napo ndio kwenyewe kwa sababu Hawa ndio Wana mchango mkubwa sana kwa kuchelewa au kuwahi kwa mizigo Yako kufika Tanzania. Hakikisha una address za kampuni yako ya usafirishaji yenye ofisi zake China mfano Guangzhou , hiyo address ndio utakayompa supplier wa mizigo uliponunua yeye ataituma mizigo kwenye hiyo shipping cargo ambao wao watakusafirishia mpaka Tanzania, itategemea umechagua mzigo wako usafirishwe kwa njia ya anga (ndege) au maji (meli). Hapa hakikisha mzigo wako supplier ameuandika jina lako vizuri kabisa pamoja na namba zako za simu kupelekea urahisi mizigo itakapofika Tanzania, pia hakikisha muuzaji anakutumia risiti ya kielektroniki ambayo utaonyesha ukienda kuchukua mzigo ukifika.

Baada ya mzigo kufika anza kuuza mzigo wako.

Kama ulikuwa na wateja ambao walikuwa wameoda mzigo, waambie mzigo umefika au  kama umeagiza kwa ajili ya kuuza dukani kwako fanya matangazo , uza na agiza mwingine na mwingine. Ni rahisi sana na inawezekana kuagiza bidhaa kutoka China.

Mawasiliano yangu ya Whatsapp ni +255626101470

Ama email: lusubilokayange@gmail.com


Comments

Popular posts from this blog

NAFASI ZA KAZI MPYA UNICEF (Re- Advertisement): Temporary Appointment - Health (Financing) Specialist P3 Tanzania

APPLY NOW Job no:   576667 Contract type:   Temporary Appointment 💥 TAZAMA NAFASI MPYA UNICEF SENIOR OPERATIONS ASSOCIATIONS Duty Station:   Dar-es-Salaam Level:   P-3 Location:   United Republic of Tanzania Categories:   Health Deadline: 10 Nov 2024 11:55 PM UNICEF works in over 190 countries and territories to save children’s lives, defend their rights, and help them fulfill their potential, from early childhood through adolescence. At UNICEF, we are committed, passionate, and proud of what we do. Promoting the rights of every child is not just a job – it is a calling. UNICEF is a place where careers are built: we offer our staff diverse opportunities for personal and professional development that will help them develop a fulfilling career while delivering on a rewarding mission. We pride ourselves on a culture that helps staff thrive, coupled with an attractive compensation and benefits package. Visit  our website  to learn more about what we ...

Tangazo la Nafasi Za Kazi Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST)

  Apply Now Apply Now/Omba sasa nafasi hizi za kazi

Tech-Driven Conservation: Protecting the Congo Basin Rainforest

The Congo Basin rainforest, the world’s second-largest tropical forest, plays a crucial role in global biodiversity and climate regulation.  Spanning over 500 million acres, it is home to diverse wildlife, including gorillas, forest elephants, and rare plant species.  Additionally, the rainforest acts as a major carbon sink, helping mitigate climate change. However, illegal logging, mining, and agricultural expansion pose significant threats to this fragile ecosystem. Technology is emerging as a powerful tool in the fight against deforestation and habitat destruction.  Advanced satellite imagery and AI-powered monitoring systems are being used to track illegal activities in real time, allowing conservationists to respond swiftly to environmental threats.  Drones are also being deployed for aerial surveillance, capturing high-resolution images to assess forest health and detect deforestation hotspots. Blockchain technology is revolutionizing supply chain transparency,...