Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Maelekezo kwa Wamiliki wa Mabasi ya Sauli na New Force: Lazima Watoe Maelezo Kabla ya Kufanyiwa Udhibiti

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imefanya kikao kilichohusisha Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani na wamiliki wa mabasi ya Sauli na New Force yaliyosababisha ajali ya tarehe 28 Machi, 2024 majira ya saa tisa na dakika arobaini na mbili (09:42) alfajiri, ambapo magari matatu yaligongana eneo la Mashamba ya Mpunga Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani katika barabara ya Morogoro. Kufuatia kikao hicho, Mamlaka imewataka wasafirishaji hao kutoa maelezo kwa maandishi kabla ya kuchukua hatua za kiudhibiti dhidi yao.

pakua taarifa kamili