Skip to main content

Ubalozi wa Tanzania Afrika Kusini wawaondoa hofu watanzania kufuatia vurugu zinazoendelea nchini humo



Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Ubalozi wake wa Afrika Kusini inapenda kuwaondoa hofu Watanzania kuwa mpaka sasa hakuna Mtanzania yeyote aliyedhurika ama kukamatwa kwa kujihusisha na vurugu na maandamano yanayoendelea katika baadhi ya miji Nchini humo kushinikiza kuachiwa kwa Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Zuma.

Serikali kupitia Ubalozi wake uliopo Nchini humo unaendelea kufuatilia na kuwasiliana kwa karibu na Viongozi wa Jumuiya mbalimbali za Watanzania waishio Afrika Kusini, Mamlaka na vyombo vya Ulinzi na Usalama ili kufahamu endapo kuna Mtanzania yeyote aliyehusishwa ama kudhurika na tukio hilo.


“Kama Serikali ya Afrika Kusini inavyoelekeza, Ubalozi wa Tanzania Afrika Kusini unawasihi Watanzania waliopo hapa kuendelea kuwa watulivu na kutojihusisha na vurugu,pamoja na maandamano yanayoendelea Nchini hapa,” Amesema Balozi Meja Jenerali (Mst) Gaudence Milanzi.


Balozi Milanzi ameongeza kuwa, kwa sasa Serikali ya Afrika Kusini imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuhakikisha vurugu hizo zinadhibitiwa kwenye maeneo hayo ili zisisambae katika maeneo mengine na kwamba Jeshi la Ulinzi la Afrika Kusini limeelekezwa kuungana na Jeshi la Polisi katika kudhibiti vurugu hizo.

Maandamano na vurugu hizo zilianza juma lililopita kupinga adhabu iliyotolewa na mahakama ya juu Nchini humo kwa Rais Mstaafu wa Taifa hilo Mhe. Jacob Zuma ya kutumikia kifungo cha miezi 15 Gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kuidharau Mahakama (Contempt of Court). Hadi sasa taarifa zinaonesha kuwa Miji mingi Nchini Afrika Kusini iko shwari na haijaathiriwa na vurugu na maandamano hayo.

Comments

Popular posts from this blog

Call for applications- Oxford Africa Conference Innovation Seed Fund

πŸ“’ Call for Applications! MUHAS students and recent graduates are invited to apply for the 2026 Oxford Africa Conference Innovation Seed Fund (ISF) in partnership with the University of Oxford. Win up to £5,000 under: 1️⃣ Nsiona Social Impact Innovation Award (£5,000) Delivered in partnership with Nsiona Impact, this award supports initiatives demonstrating measurable and scalable social impact across Africa. πŸ”— Apply: https://lnkd.in/dmm4gr_r 2️⃣ Oxford University Innovation (OUI) Entrepreneurial Prize (£5,000) Proudly supported by Oxford University Innovation, this prize backs an outstanding founder building a venture rooted in Africa’s realities and designed for durable impact. πŸ”— Apply: https://lnkd.in/dmm4gr_r ✅ Open to current students and recent graduates (within one year) of African universities ✅ £5,000 in non-dilutive funding ✅ Finalists will pitch physically or virtually in May 2026 πŸ—“ Deadline: 28 February 2026 #MUHAS #OxfordAfricaConference #Innovation #AfricaLedSolutions ...

FULLY FUNDED ELECTIVE ROTATION (USA) πŸ‡ΊπŸ‡Έ OPPORTUNITIES

🚨 CALL FOR APPLICATIONS – FULLY FUNDED ELECTIVE ROTATION (USA) πŸ‡ΊπŸ‡Έ Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS), in collaboration with Dartmouth Geisel School of Medicine, invites MD4 and MD5 female students to apply for a Fully Funded Elective Rotation in Emergency Medicine and Internal Medicine. πŸ“ Location: New Hampshire, USA πŸ“… Clinical Placement: 10th September – 30th October 2026 πŸŽ“ Coverage: Tuition, accommodation, airfare & meals πŸ‘©‍⚕️ Slots Available: 2 ✨ If you have a strong academic record (GPA 3.5+), an A grade in Emergency/Internal Medicine, and a passion for pursuing a career in these specialties — this is your opportunity to gain international clinical exposure at a world-class institution. πŸ“© Submit: • One-page personal statement • Updated CV (max 2 pages) • Valid US Visa or proof of ability to obtain one πŸ“§ Send applications to: icu@muhas.ac.tz muhas.convocation@gmail.com ⏰ Deadline: 14th March 2026, 1700 hours EAT Don’t miss this prestigious opport...