Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Rais Samia afanya uteuzi tena, Hamad NHC, Mchechu Hazina?

 Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi kama ifuatavyo:-

Amemteua Bw. Nehemia Kyando Mchechu, kuwa msajili wa Hazina. Kabla ya uteuzi huo Bw. Mchechu alikuwa Mkurugenzi MKUU wa shirika la nyumba la Taifa (NHC). Bw. Mchechu anachukua nafasi ya Bw. Mgonya Benedicto ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Pia amemteua Bw. Hamad Abdalah kuwa MKURUGENZI Mkuu wa SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC), Kabla ya uteuzi huo , Bw. Abdallah alikuwa Mkurugenzi mtendaji wa GIMCOAFRICA Limited na anachukua nafasi ya Bw. Mchechu ambaye ameteuliwa kuwa msajili wa Hazina.

Zaidi Rais Samia amemteua Bw. Mussa Mohammed Makame, kuwa Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la maendeleo ya petroli Tanzania (TPDC), na pia ni mshauri mwelekezi wa masuala ya mafuta na gesi nchini Tanzania. Bw. Makame anachukua nafasi ya Dkt. James Mataragio ambaye atapangiwa kazi nyingine

Uteuzi huu ni kuanzia tarehe 24 Februari 2023.